Hifadhi ya Taifa ya Gombe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Gombe)
Sokwe wa hifadhi ya Gombe.
Sokwe anayekula.
Sokwe katika Hifadhi ya Gombe.

Hifadhi ya Taifa ya Gombe inapatikana kwenye mto Gombe, magharibi mwa Mkoa wa Kigoma, Tanzania.

Ni hifadhi ndogo kuliko zote nchini ikiwa na kilometa za mraba 52 tu, lakini ina umaarufu mkubwa unaotokana na kivutio chake kikubwa ambacho ni sokwe.

Iko umbali wa kilometa 16 kaskazini kwa mji wa Kigoma, ambao ni makao makuu ya Mkoa wa Kigoma.

Hifadhi hii ulianzishwa mwaka wa 1968, na ni ukanda mwembamba wa msitu wa mlimani unaokatizwa na miteremko mikali inayoingia katika mwambao wa mashariki wa Ziwa Tanganyika. Eneo hilo linajulikana na mabonde ya mwinuko, na mimea ya misitu inayotoka kati ya majani hadi mianzi ya milima hadi msitu wa mvua ya kitropiki.

Gombe ni miongoni mwa makazi machache yaliyosalia ya sokwe duniani. Hifadhi hii ilipata hasa umaarufu baada ya mtafiti wa tabia ya sokwe duniani, Jane Goodall kufanya utafiti juu ya maisha na tabia za sokwe wa Gombe kwa miaka 40 na kuandika vitabu kadhaa kuhusu viumbe hao. Jamii ya sokwe ya Kasakela, iliyo katika vitabu na hati kadhaa, huishi katika hifadhi hiyo.

Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na kima wenye mikia myekundu na kima wa bluu.

Wanyama wa jamii ya paka, kama chui na simba hawapo katika hifadhi hii na hivyo kuifanya kuwa salama kwa safari za miguu.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni wakati wa kiangazi, Julai-Oktoba kwa sababu sokwe hawapendi kutembea nyakati za mvua. Chombo cha usafiri kitumikacho kwenda hifadhi ya Gombe ni mashua.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Majarida ya hifadhi za Taifa Tanzania

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kigoma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hifadhi ya Taifa ya Gombe kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.