Go-Kashiwabara
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Go-Kashiwabara (19 Novemba, 1464 – 19 Mei, 1526) alikuwa mfalme mkuu wa 104 (Tenno) wa Japani. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Katsuhito. Tarehe 16 Novemba, 1500 alimfuata baba yake, Go-Tsuchimikado, na kuwa mfalme hadi kifo chake. Aliyemfuata ni mwana wake, Go-Nara.

