Fransisko wa Fabriano

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jumba la Meya wa Fabriano, lililojengwa wakati wa utoto wa Fransisko Venimbeni.

Fransisko Venimbeni wa Fabriano (2 Septemba 1251 - 22 Aprili 1322) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo kutoka Fabriano (Marche, Italia).

Mapema alianza kuheshimiwa kama mwenye heri. Hatimaye Papa Pius VI alithibitisha uhalali wa heshima hiyo tarehe 1 Aprili 1775.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Kisha kumaliza masomo yake ya sayansi za jamii na falsafa, alijiunga na Wafransisko mwaka 1267, akajikita katika masomo ya teolojia, uandishi na utume katika mji wake asili na maeneo ya kandokando.

Alikuwa wa kwanza kuipatia konventi ya shirika lake maktaba kubwa.

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake ("Chronica Marchiæ et Fabriani", "De veritate et excellentiâ Indulgentiæ S. Mariæ de Portiuncula", "Opusculum de serie et gestis Ministrorum Generalium", "Ars Prædicantium", mbali na "Hotuba" na vitabu vingine) yamepotea karibu yote.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.