Fransisko Antoni Fasani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Fransisko Antonio Fasani)

Fransisko Antoni Fasani (Lucera 6 Agosti 1681 - Lucera 29 Novemba 1742) alikuwa padri wa utawa wa Ndugu Wadogo Wakonventuali kutoka Italia Kusini.

Msomi mkubwa, alipenda sana kuhubiri na kufanya toba, pamoja na kuhurumia fukara kwa kuwapa hata mavazi yake.

Alitangazwa na Papa Pius XII kuwa mwenye heri tarehe 15 Aprili 1951, halafu tarehe 13 Aprili 1986 Papa Yohane Paulo II alimtangaza kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.