Fransiska wa Roma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Fransiska wa Roma (kwa Kiitalia Francesca Romana; 13849 Machi 1440) alikuwa mtawa kutoka Roma, Italia.

Ametambuliwa na Kanisa Katoliki chini ya Papa Paulo V kuwa mtakatifu kuanzia mwaka wa 1608.

Tarehe ya kifo chake, yaani 9 Machi ndiyo sikukuu yake[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Fransiska alizaliwa katika mji wa Roma, Italia, mwaka 1384.

Aliolewa mapema mwaka 1396, akazaa watoto watatu. Katika miaka 40 ya ndoa yake alijitokeza kama mke na mama bora. Alijulikana sana kwa moyo wake wa ibada, unyenyekevu, upole, uvumilivu na kujitoa kwake mhanga kuwasaidia maskini. Aliishi nyakati ngumu, hivyo aliwapatia mali yake, na kuuguza wagonjwa.

Mwaka 1425 alianzisha Shirika la Waoblati waliofuata Kanuni ya Mt. Benedikto na baada ya kifo cha mumewe akajiunga nao. Alifariki dunia mwaka 1440.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.