Frank Yallop

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uwanja wa San Jose Earthquakes:ambapo Yallop alishinda taji mbili ya Ligi Kuu Ya Soka ya Marekani
Frank Yallop
Maelezo binafsi
Jina kamili Frank WalterYallop
Tarehe ya kuzaliwa 4 Aprili 1964
Mahala pa kuzaliwa    Watford, Uingereza
Urefu 1.80m
Nafasi anayochezea Difenda
Maelezo ya klabu
Klabu ya sasa San Jose Earthquakes (kocha mkuu)
Klabu za vijana
1982–1983 Ipswich Town FC
Klabu za ukubwani
Miaka Klabu
1983–1996
1995
1996–1998
Ipswich Town F.C
Blackpool F.C.
Tampa Bay Mutiny
MetroStars
Timu ya taifa
1990–1997 Ilikuwa Kanada

* Magoli alioshinda

Frank Yallop (alizaliwa Watford, 4 Aprili 1964) ni mchezaji wa kandanda wa Kanada aliyezaliwa Uingereza. Yeye ni kocha mkuu wa timu ya San Jose Earthquakes katika ligi kuu ya Marekani.

Yallop alicheza kandanda sana kama mchezaji nchini Uingereza, alicheza miaka 13 akacheza mechi 300 akiwa timu ya Ipswich Town. Wakati huu alicheza misimu mitatu katika Ligi Kuu ya Uingereza. Alicheza,pia,katika timu ya Tampa Bay Mutiny na akacheza mara 52 katika timu ya taifa ya Kanada.

Wasifu wake wa Uchezaji[hariri | hariri chanzo]

Klabu[hariri | hariri chanzo]

Ingawa alikua katika mji wa Vancouver,Yallop alicheza kandanda yake kwa takriban miaka 20 nchini Uingereza na Marekani. Katika mwaka wa 1983,akiwa umri wa miaka 19,Yallop alitia saini mkataba na Ipswich Town,timu ambayo angechezea mechi 385 (katika mashindano yote), huku akifunga mabao 8. Alipokuwa Ipswich,alicheza katika timu hiyo na mwenzake kutoka Kanada , Craig Forrest.

Baada ya kuwa mchezaji kwa muda mrefu huko Uingereza ,Yallop alirudi Amerika Kaskazini katika mwaka wa 1996. Mwaka huo, alitia saini mkataba na Ligi Kuu ya Soka na akawa nambari 57 kwa jumla katika timu ya Tampa Bay Mutiny katika orodha ya kwanza katika timu hiyo. Baada ya misimu mitatu katika timu hiyo,Yallop alistaafu kutoka uchezaji wa soka katika mwisho wa msimu wa 1998.

Kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Yallop alikosa kucheza katika Shindano la Kombe la Dunia la 1986 lenye Kanada ilihitimu kucheza(hawajawahi hitimu kucheza katika jingine).Yallop alicheza katika mechi yake ya kwanza akiwa timu ya taifa akiwa umri wa miaka 26 katika Shindano la Amerika Kaskazini(Mei 1990) dhidi ya Marekani. Kwa kuwa mechi hiyo haikuwa rasmi,mechi yake ya kweli ya kwanza ilikuwa katika Shindano lilo hilo baada ya siku chache dhidi ya Mexico. Alichezea Kanada mechi 52,akikosa kufunga bao lolote. Alicheza katika mechi 27 za kuhitimu kucheza katika Shindano la Kombe la Dunia. Mechi yake ya kimataifa ya mwisho ilikuwa dhidi ya Costa Rica katika mwezi wa Novemba 1997.

Wasifu wa Kocha[hariri | hariri chanzo]

Yallop alianza kazi ya kocha katika mwaka wa 1998 na timu ya Marekani, Project-40,akichukua timu hiyo katika ziara ya mechi tano nchini Uingereza. Kufuatia ziara hiyo, akawa kocha msaidizi kwa Tampa Bay Mutiny. Katika mwaka wa 2000, akawa msaidizi mkuu wa kocha wa timu ya DC United akiwa chini ya Thomas Rongen.

Katika mwaka wa 2001, Yallop aliajiriwa kama kocha mkuu wa San Jose Earthquakes,siku mbili tu kabla ya Orodha Kuu ya Ligi kuandikwa.Yallop aliajiri wachezaji Jeff Agoos,Landon Donovan,Dwayne DeRosario,Manny Lagos,Ramiro Corrales na Ronnie Ekelund, na vilevile kocha msaidizi Dominic Kinnear. Katika mwaka wake wa kwanza, Yallop aliongoza San Jose Earthquakes na kushinda taji lao la kwanza la Ligi Kuu ya Soka.

Katika mwaka wa 2003,the Earthquakes, chini ya uongozi wa Yallop, alikuwa na uwezo wa kushinda Ligi Kuu ya Soka kwa mara ya pili. Katika mwaka wa 2004, licha ya kuwa bado na mwaka mmoja umebaki kwenye mkataba wakeo, Yallop aliondoka klabu ya Earthquakes ili kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Kanada. Katika mwaka wa 2005,aliongezwa kwa orodha ya wale maarufu sana katika soka nchini Kanada.

Yallop alituzwa kama Kocha bora katika Ligi Kuu ya Soka Marekani,huu ulikuwa mwaka wa 2001.Akiwa mchezaji alituzwa natimu yake ya Mutiny kama Difenda wa mwaka katika miaka ya 1997 na 1998.

Mnamo 7 Juni 2006, Yallop alijiuzulu kama kocha wa timu ya taifa ya soka ya Kanada, akatangazwa kama kocha mpya wa Los Angeles Galaxy. Tarehe 4 Novemba 2007,ilitokea kuwa Yallop aliajiriwa kama kocha mkuu wa San Jose Earthquakes tena katika msimu wa 2008.Ruud Gullit,Mholanzi maarufu, alichukua nafasi yake.

Tuzo[hariri | hariri chanzo]

Kama mchezaji[hariri | hariri chanzo]

  • Ligi Ya Soka Ya Daraja la Pili: 1
1992

Kama meneja[hariri | hariri chanzo]

  • Kombe la Ligi Kuu ya Soka :2
2001, 2003
  • Kocha wa Mwaka katika Ligi Kuu Ya Soka :1
2001

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. ^ Rekodi katika mashindano ya FIFA - FIFA Archived 13 Februari 2010 at the Wayback Machine.
  2. ^ SI.com - Soka - Jonah Freedman: Earthquakes wamwajiri Yallop kutoka Galaxy - Jumatatu Novemba 5, 2007 10:14AM
  3. ^ Tovuti kamili ya Earthquakes LLC - News Archived 21 Mei 2009 at the Wayback Machine.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]