Mshambuliaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Winga Nani akijaribu kufunga goli kwa kumkwepa beki Philipp Lahm (kulia).
Mshambuliaji (10, jezi nyekundu) kamtoka beki (16, jezi nyeupe) na yupo tayari kupiga shuti kujaribu kufunga. Golikipa naye atajitahidi kuzuioa goli kwa kutokuruhusu mpira usivuke mstari wa goli.

Mshambuliaji (kutoka kitenzi “kushambulia”) ni mchezaji wa nafasi ya mbele anayetakiwa kufunga goli katika michezo mbalimbali kama vile: mpira wa miguu, raga, hoki ya ugani. Hivyo anacheza karibu na goli la timu pinzani akiwa na majukumu makubwa ya kufungia timu yake.

Nafasi yake uwanjani na kazi ndogo ya ukabaji awapo michezoni humaanisha mshambuliaji ndiye wa kufunga magoli mengi zaidi kwa niaba ya timu nzima na wachezaji wenzake.

Mfumo wa kisasa kwa ujumla hutumia mshambuliaji mmoja mpaka watatu; kwa mfano, mfumo uliozoeleka wa 4–2–3–1 hutumia mshambuliaji mmoja.[1][2][3]

Mshambuiliaji wa kati[hariri | hariri chanzo]

Mshambuliaji wa Brazili Ronaldo akipiga shuti kuelekea golini. Ni mshambuliaji anayeweza kufanya majukumu mengi akiwa uwanjani, ameshawishi washambuliaji wengi waliocheza baada yake.[4]

Jukumu la msingi la mshambuliaji wa kati ni kufunga idadi kubwa ya magoli kwa niaba ya timu yake. Anaweza kutumika pia katika kupokea mipira mirefu inayopigwa kutoka golini kwake au kukaba mipira ikiwa eneo la ulinzi wa timu. Washambuliaji wa kati mara nyingi hucheza juu ya mshambuliaji wa pili au viungo washambuliaji na hufanya majukumu yote ya kumiliki mipira nje ya kisanduku cha timu pinzani. Majukumu ya mshambuliaji wa kati mara nyingine hubadili baina yao na viungo washambuliaji hasa kwenye mfumo wa 4–3–1–2 au 4–1–2–1–2. Katika lugha ya kiingereza, neno "target man"' hutumika kumaanisha aina fulani ya mshambuliaji mwenye majukumu ya kupokea na kumiliki mipira ya juu na kusambaza pasi kutengeneza nafasi kwa wachezaji wenzake kufunga.[5] Wachezaji wengi wa kiwango hii huwa warefu wenye maumbo makubwa na wenye nguvu sana. Mfumo wa nambari ulipoanzishwa mwaka 1933 katika fainali za kombe la FA nchini Uingereza, mmoja kati ya washambuliaji wawili wa kati Dixie Dean wa klabu ya Everton F.C. alivaa jezi nambari 9, alikua mchezaji mwenye nguvu aliyeweka rekodi ya magoli mengi katika msimu wa 1927–28. Nambari hiyo tangu hapo imekuwa ikitumika kwa mshabuliaji wa kati.[6]

Mshambuliaji wa ndani[hariri | hariri chanzo]

mfumo wa 2–3–5: washambuliaji wa ndani (rangi nyekundu) humzunguka mshambuliaji wa kati.

Nafasi ya mshambuliaji wa ndani ulitumika sana katika karne ya 19 na nusu karne ya 20. Washambuliaji hawa ni wasaidizi wa washambuliaji wa kati katika kukimbia na kutafuta nafasi katika ulinzi wa timu pinzani. Jukumu lao linafanana kwa kiasi kikubwa na jukumu la viungo washambuliaji au mshambuliaji nambari mbili katika soka la kisasa.

WM Formation: washambuliaji wa ndani (rangi nyekundu) hucheza zaidi katika nafasi zilizotolewa na huwasaidia washambuliaji wa kati.

Katika mfumo wa mwanzo wenye muundo wa piramidi wa 2–3–5 washambuliaji wa ndani huwazunguka washambuliaji wa kati katika pande zote. Katika mfumo uliobadilishwa wa "WM", washambuliaji wa ndani wamerudishwa nyuma kucheza kama viungo washambuliaji.

Washambuliaji wa nje[hariri | hariri chanzo]

mfumo ulioanzishwa na Vittorio Pozzo kwa jina la Metodo kuanzia miaka ya 1930 ilihusisha winga wanaoshambulia

Mshambuliaji wa nje hucheza kama mshambuliaji wa juu katika upande wa kulia na kushoto mwa uwanja, nafasi hizi zipo katika mfumo wa 2–3–5 au zenye mfanano huu. Kutokana na mabadiliko mengi yanayotokea katika soka, wing'a wameshushwa nyuma kucheza kama viungo, mabadiliko haya yamesababisha nafasi a washambuliaji wa nje kuwa historia tu.

Majukumu ya washambuliaji wa nje yanajumuisha:

  • Kufunga magoli: Chaguo lao la kwanza mar azote ni kupiga mashuti wakipata mipira, chaguo la pili ni kutoa pasi kutengeneza nafasi za kufunga.
  • Kutoa pasi: Wakiwa katika nafasi ambayo sio rahisi kufunga, hutoa pasi katikati ya eneo la penalti ili washambuliaji wa kati wafunge.

Kwa sababu ya majukumu haya sifa muhimu za wachezaji wa nafasi hii ni pamoja na:

  • Uwezo wa kukokota mipira na kupiga chenga
  • Kasi na uwezo wa kutengeneza mashambulizi ya kushtukiza.

Wing'a[hariri | hariri chanzo]

Cristiano Ronaldo alicheza kama winga.

wing'a ni aina ya mshambuliaji anayecheza pembezoni mwa uwanja. Wanajumuishwa katika safu ya washambuliaji kutokana na nafasi hiyo kuwa "washambuliaji wa pembeni" kabla ya mabadiliko ya soka. Hata na hivyo, katika mfumo wa 4–4–2 wenye asili ya Uingereza, wing'a huchukuliwa kama sehemu ya kiungo.

Ni jukumu la wing'a kumshinda na kupita ulinzi wa beki wa pembeni na kucheza pasi a krosi kwa washambuliaji wa kati au kupunguza umbali walipo na goli na kupiga mashuti kujaribu kufunga. Mara nyingi huwa ndio wachezaji wenye kasi zaidi katika timu na wenye mbinu nzuri na ujuzi wa kukokota mipira. Katika soka la Uholanzi, Uhispania na Ureno, majukumu ya kiulinzi ya wing'a ni kuzuia beki wa pembeni wasipande kuongeza mashambulizi wakati wote timu yake inaposhambuliwa.

Mohamed Salah akiwa anacheza kama wing'a wa kulia, nafasi inayompa faida ya kugeuka kuingia ndani na kutumia kwa ufasaha mguu wa kushoto anaoutumia sana

Katika soka la Uingereza na nchi nyingi kaskazini mwa Ulaya, viungo wa pembeni huwa na majukumu ya kushuka kwa kiasi kikubwa mpaka eneo la bendera ya kona kama beki wake atamuhitaji kufanya hivyo. Haya ni majukumu makubwa sana kwa wachezaji wenye kiwango cha ushambuliaji kama Joaquín Sánchez, Cristiano Ronaldo au Ryan Giggs na John Barnes wanaokosa uwezo wa kurudi kusaidia ulinzi. Kadri umri wa wachezaji hawa unavyoenda, mara nyingi hubadilishwa na kucheza kama nambari 10 katikati ya viungo wa kati na washambuliaji. Mfano mzuri ni klabu ya Inter Milan ilipokuwa inamtumia mkongwe Luís Figo nyuma ya mshambuliaji moja au wawili kama mshambuliaji nambari mbili au kiungo mshabuliaji.[7]

Nambari 9 hewa[hariri | hariri chanzo]

mshambuliaji wa klabu ya FC Barcelona Lionel Messi amekuwa miongoni mwa wachezaji wa hivi karibuni aliyecheza nambari 9 hewa kwa mafanikio makubwa.

Nambari 9 hewa, ana mfanano fulani na kiungo mshambuliaji wa juu, nafasi hii inahusisha mshambuliaji mmoja anayeshuka kwa kiasi kikubwa katika nafasi ya kiungo. Lengo kuu ni kutengeneza nafasi katika safu ya ulinzi ya timu pinzani, ikiwa ni kulazimisha beki wa kati mmoja kumfuata nambari 9 kwa nia ya kumkaba.

Istilahi hiyo imetokana na nambari 9 iliyozoeleka, kwa kawaida nambari 9 ni mashambuliaji wa juu kabisa katika timu, anategemewa kuwa katika mstari wa safu ya ulinzi wa timu pinzani kwa muda mwingil.[8]

sifa muhimu za nambari 9 hewa ni sawa na zile za mshambuliaji wa juu wa mwisho: uwezo wa kipekee wa kukokota mipira kupenya katika nafasi zilizoachwa wazi, upigaji wa pasi fupi na uwezo wa kuona nafasi za magoli.

Mchezaji wa kwanza kucheza kama nambari 9 hewa katika fainali za Kombe la Dunia ni Juan Peregrino Anselmo katika kikosi cha timu ya taifa ya Uruguay, ijapokuwa hakucheza katika mechi dhidi ya Argentina katika fainali za Kombe la Dunia za mwaka 1930 kwa sababu ya majeraha. Matthias Sindelar alikuwa nambari 9 hewa katika kikosi cha Austria kilichojulikana zaidi kwa jina la Wunderteam mwaka 1934.[9] Namba 9 hewa ilitumika sana na timu ya taifa ya Hungaria miaka ya 1950 mshambuliaji Nándor Hidegkuti akicheza katika nafasi hiyo.

Klabu ya Roma chini ya kocha wao Luciano Spalletti walimtumia Francesco Totti, aliyecheza kama kiungo mshambuliaji mbele juu na kutoka na mfumo wa "4–6–0";[10] hii ilisababisha ushindi wa michezo 11 mfululizo.

Katika mashindano ya UEFA Euro ya 2012, timu ya taifa ya Uhispania chini ya kocha Vicente del Bosque, japo mara kadhaa alitumia mshambuliaji halisi Fernando Torres, walitumia nambari 9 hewa iliyochezwa na Cesc Fàbregas katika badhi ya michezo ikijumuisha mchezo wa finali. Mwishoni mwa mwaka 2012, matumizi ya nambari 9 hewa yalishika hatamu na klabu nyingi zilitumia mfumo unaohusisha nafasi hii kwa kiasi kikubwa. Lionel Messi wa klabu ya Barcelona amekua mchezaji mwenyemafanikio sana katika miaka ya hivi karibuni akicheza kama nambari 9 hewa, kwanza chini ya kocha Pep Guardiola na baadae mrithi wake Tito Vilanova.[11]

Njia moja ya kuzuia mfumo unaotumia nambari tisa hewa ni kusababisha msongamano katika safu ya kiungo kwa kuongeza wachezaji wengi zaidi eneo la kiungo wakabaji ili kupunguza uwezo wa kutengeneza nafasi za magoli, kocha José Mourinho anafahamika kwa mkakati wa "kupaki basi" iliofanikiwa kuzuia mfumo unaotumia nambari 9 hewa.[8]

Timu shambulizi[hariri | hariri chanzo]

Messi, Luis Suárez (kwenye picha) na Neymar, waliunda kundi shambulizi iliyovunja rekodi kwa jumla ya magoli 131 katika msimu mmoja ndani ya Barcelona.[12]

Timu shambulizi ni mjumuiko wa wachezaji wawili au zaidi wanaounda safu ya ushambuliaji ya timu ya kwanza ya klabu yoyote. Historia ya soka imekuwa njia wachezaji wa namna hii kwa kiasi kikubwa sana. Ikihusisha wachezaji watatu hufanya kazi kwa muundo wa pembe tatu, hii huongeza ufanisi na urahisi wa kufunga. Ikiwa na wachezaji wanne huwa na chaguzi nyingi zaidi.

Mshambuliaji ni lazima awe mnyumbulifu na uwezo wa kubadili majukumu kwa wakati wowote atakapotakiwa kufanya hivyo.

Moja kati ya kundi shambulizi lililopata mafanikio sana ni lile la washambuliaji watatu wa klabu ya Barcelona Lionel Messi, Luis Suárez na Neymar. Walifunga kwa wastani wa goli moja ndani ya dakika 45– magoli mawili kwa mechi moja.[13]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Cox, Michael. "FIFA's 289-page Technical Report on the 2010 World Cup – in 15 points", 3 September 2010. Retrieved on 17 August 2013. Archived from the original on 2018-11-04. 
  2. Cox, Michael. "Is Barcelona's alternative shape really a 4–2–4?", 19 March 2010. Retrieved on 17 August 2013. Archived from the original on 2019-02-21. 
  3. Cox, Michael. "Teams of the Decade #5: Roma, 2007", 5 March 2010. Retrieved on 17 August 2013. Archived from the original on 2019-07-26. 
  4. "Ronaldo at 40: Il Fenomeno’s legacy as greatest ever No 9, despite dodgy knees", 17 September 2016. 
  5. "Target Man Definition In Soccer - Meanings & Examples From SportsLingo.com". (en-US) 
  6. Khalil Garriot (21 June 2014). "Mystery solved: Why do the best soccer players wear No. 10?". Yahoo. Iliwekwa mnamo 19 May 2015.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  7. "Positions guide: Wide Midfield", BBC Sport, 1 September 2005. Retrieved on 21 June 2008. 
  8. 8.0 8.1 "Football Tactics for Beginners: The False 9". The False 9 – Football Tactics Simplified. Iliwekwa mnamo 17 January 2017.  Check date values in: |accessdate= (help)
  9. "Building the Ideal False Nine for the Modern Era". Bleacher Report. 16 May 2013. Iliwekwa mnamo 14 May 2014.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  10. "Great Team Tactics: Francesco Totti, Roma and the First False Nine". Bleacher Report. 6 December 2012. Iliwekwa mnamo 14 May 2014.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  11. "5 The football tactical trends of 2012". Retrieved on 8 January 2019. 
  12. "Messi, Suárez and Neymar Jr end season with 131 goals". Retrieved on 2 August 2019. 
  13. "MOTD Kickabout - 7 of MSN's most mind-boggling stats". Retrieved on 2 August 2019. 
Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu zaidi kuhusu Mshambuliaji kama historia yake, uenezi au kanuni zake?
Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.