Didake

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta

Didake (yaani Mafundisho) ya Mitume Kumi na Wawili ni kimojawapo kati ya vitabu vya kale zaidi vya Ukristo, ambavyo viliandikwa na Mababu wa Kanisa na vinapatikana nje ya Biblia.

Kinakadiriwa kiliandikwa kati ya mwaka 70 na 150 BK katika mazingira ya Syria. Mwandishi wake hajulikani.

Kitabu kilipatikana tena mwaka 1873 huko Yerusalemu.

Lengo lake ni malezi ya Kikristo, yaani kupokeza mafundisho ya Mitume kwa katekesi juu ya maadili inayotofautisha "njia ya mauti" na "njia ya uzima", ikiwa na orodha ya vilema na maadili mema, ikifuatwa na matini ya liturujia na taratibu kuhusu ubatizo na ekaristi.

[hariri] Tafsiri ya Kiswahili

  • Didakè yaani Mafundisho ya Mitume Kumi na Wawili na Waraka wa Mt. Klementi kwa Wakorinto, tafsiri ya B. Santopadre n.k. – ed. E.M.I. – Bologna (Italia) 1990 – ISBN 88-307-0321-4

[hariri] Marejeo

  • Audet, Jean-Paul, La Didache, Instructions des Apôtres, J. Gabalda & Co., 1958.
  • Draper, Jonathan, ed. 1996. The Didache in Modern Research (Leiden, New York and Cologne)
  • Holmes, Michael W., ed., The Apostolic Fathers: Greek Texts and English Translations, Baker Academic, December 1, 1999. ISBN 978-0-8010-2225-8
  • Lightfoot, Joseph Barber, et al., Apostolic Fathers, London: Macmillan and Co. 1889.

[hariri] Viungo vya nje

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine