Kua

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Coua)
Kua
Kua mkubwa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Cuculiformes (Ndege kama kekeo)
Familia: Cuculidae (Ndege walio na mnasaba na kekeo)
Nusufamilia: Phaenicophaeinae (Ndege wanaofanana na malkoha)
Jenasi: Coua
Schinz, 1821
Ngazi za chini

Spishi 11:

Kua (kutoka Kimalagasy: koa) ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Coua katika nusufamilia Phaenicophaeinae ya familia Cuculidae. Pengine wanaainishwa katika nusufamilia yao Couinae pamoja na kekeo-ardhi wa Asia (Carpococcyx). Jenasi pekee ya Bara la Afrika inayoainishwa katika Phaenicophaeinae ni Ceuthmochares (ukiki). Kua ni ndege wa Madagaska wanaofanana na kekeo. Wana mkia mrefu na miguu mirefu. Kidole cha tatu cha miguu yao kinaweza kukabili mbele au nyuma. Rangi kuu ni kijivu na/au buluu na wana ngozi tupu kuzunguka macho yenye rangi buluu. Kua hula mbegu, matunda madogo, wadudu na wanyama wadogo kama mijusi na vigeugeu. Kinyume na kekeo, kua hulijenga tago lao lenyewe. Jike huyataga mayai meupe 1-3 (2 mara nyingi zaidi).

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za kabla ya historia[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]