Chuo Kikuu cha Mekelle

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Chuo Kikuu cha Mekelle
MahaliMek'ele, Ethiopia
Tovutihttp://www.mu.edu.et/

Chuo Kikuu cha Mekelle kiko Kaskazini mwa Ethiopia (Mekelle au Mek'ele, Tigray), katika umbali wa kilomita 783 kutoka mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa. Chuo hiki kina Kampasi tatu ndani ya mji wa Mek'ele, kampasi ya Endayesus (Kilimo cha Ardhi Kavu na Usimamizi wa Maliasili, Sayansi za kikompyuta Sci, Uhandisi na sayansi ya kompyuta, Sayansi ya Utibabu wa Wanyama),kampasi ya Adi Haki (Sheria na Utawala Bora, Lugha na ubinadamu, Biashara na Uchumi), na kampasi ya Aida (Chuo cha Sayansi ya Afya). Kampasi ya nne iko chini ya ujenzi katika Kelamino kama chuo cha Sayansi ya utibabu wa Wanyama. Chuo Kikuu cha Mekelle kilianzishwa Mei mwaka wa 2000 na Serikali ya Ethiopia (Baraza la Mawaziri, Kanuni No 61/1999 ya Ibara ya 3) kama taasisi elimu yenye ina sheria zake kibinafsi. Shule hili lilimiliki jina lake utoka malkia Mekell.[onesha uthibitisho] Kuunganisha vyuo viwili ndiko kuliumba chuo hiki kikuu: Chuo cha Mekelle cha Biashara Mekelle na chuo cha Mekelle. Vyuo hivi viwili vina maendeleo ya kihistoria na uhamishaji.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Chuo Kikuu cha Mekelle kilianza maisha mwaka wa 1993 kama chuo cha kilimom cha ardhi kavu ambacho mahali pa kudumu katika Mek'ele baada ya kuhamishwa mara kadhaa. Wakati wa serikali ya zamani, Chuo awali kilipangiwa kuhamishwa Seleh Leha, katika Northwestern Tigray. Lakini, kutokana na sababu nyingi, ilianzishwa kwanza katika Chuo Kikuu cha Asmarakama idara, lakini baadaye kilihamishwa Agarfa, kusini mwa Ethiopia, wakati Derg kuhamisha chuo kikuu cha Asmara mwaka 1990 kutokana na migogoro ya kisiasa wakati huo. Mwaka wa 1991, baada ya zaidi ya mwaka, Chuo kikuu cha Asmara kilirudi Asmara na Shule ya Kilimo cha Ardhi kavu ilihamia Chuo kikuu cha Alamaya. kwa muda mfupi Mwaka wa 1993, Chuo cha Kilimo katika Ardhi kavu kilihamishwa, Mek'ele kama Chuo cha Kilimo cha artdhi kavu na Usimamizi wa Maliasili, na kuata makazi ya kudumu katika kampasi ya Endayesus , ambayo imekuwa kituo cha jeshi tangu wakati wa Mfalme Menelik.

Baada ya wanakabiliwa na changamoto, Chuo cha kilimo katika ardhi kavu kliianza na digrii tatu mwaka wa 1993 pamoja na wanafunzi 42 . Baada ya miaka miwili, wa Kitivo cha Sayansi na Teknolojia kilianzishwa katika kampasi hii, vitivo hivi viwili vilipandishwa cheo na kuwa Chuo kikuu na Chuo cha Mekelle. Vile vile Kitivo cha sheria kilianza kwa kukubali wanafunzi wa diploma katika mpango wa elimu ya kuendelea .

Cho Kikuu cha Mekelle ni moja ya Vyuo vikuu 13vya kidunia nchini Ethiopia. Katika chuo kikuu cha Mekelle , kuna vitivo saba na idara 44.

Vyuo na vitivo[hariri | hariri chanzo]

Kwa sasa, Chuo Kikuu hicho kina vitivo vifuatavyo:

  • Chuo cha Kilimo Katika Ardhi Kavu
  • Chuo cha Biashara na Uchumi
  • Chuo cha Ubinadamu na Lugha.
  • Chuo cha Sayansi ya Mazingra na Kikompyuta
  • Chuo cha Sheria na Utawala
  • Taasisi ya sayansi ya Matibabu
  • Chuo cha Sayansi ya Utibabu wa Wanyama
  • Chuo cha Sayansi ya Afya
  • Chuo cha Uhandisi na Teknolojia