Christiaan Eijkman
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Christiaan Eijkman (11 Agosti, 1858 – 5 Novemba, 1930) alikuwa daktari kutoka nchi ya Uholanzi. Hasa alichunguza ugonjwa wa beriberi na sababu zake. Mwaka wa 1929, pamoja na Frederick Hopkins alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.

