Shashi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Buphagidae)
Shashi
Shashi domo-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Muscicapoidea (Ndege kama shore)
Familia: Buphagidae (Ndege walio na mnasaba na shashi)
Lesson, 1828
Jenasi: Buphagus
Brisson, 1760
Ngazi za chini

Spishi 2:

Shashi au wadondoakupe ni ndege wadogo kiasi wa jenasi Buphagus, jenasi pekee katika familia Buphagidae. Wanatokea Afrika tu. Ndege hawa wana rangi ya kijivu au kahawa juu na nyeupe au njano kahawia chini. Hula kupe na vidusia wengine kwa ngozi ya wanyama pori wakubwa na ya ng'ombe pia. Hula vidusia vilvyojaa damu hasa na pia damu na tishu za wenyeji. Kwa hivyo wanasababisha vidonda viendelee kuwa wazi na tunaweza kusema kwamba shashi wenyewe ni vidusia. Huliweka tago lao kwa tundu mtini au pengine ukutani. Jike huyataga mayai 2-5.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]