Cherimiyo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bias)
Cherimiyo
Cherimiyo rangi-mbili
Cherimiyo rangi-mbili
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Corvoidea (Ndege kama kunguru)
Familia: Platysteiridae (Ndege walio na mnasaba na bwiru)
Jenasi: Bias Lesson, 1831

Megabyas J. Verreaux & E. Verreaux, 1833

Spishi: Angalia katiba.

Cherimiyo ni ndege wadogo wa jenasi Bias na Megabyas katika familia Platysteiridae wanaotokea Afrika kusini kwa Sahara. Zamani waliainishwa katika familia Muscicapidae. Labda Bias ina mnasaba zaidi na milali (Prionopidae).

Kila jenasi ina spishi moja tu. Dume la spishi zote mbili ni mweusi juu na mweupe chini, lakini cherimiyo-mbwigu ana kishungi na koo lake ni jeusi. Jike ni kahawia au kahawiachekundu. Cherimiyo hula wadudu na hulijenga tago lao kwa majani, uvumwani na utando wa buibui na kwa umbo wa kikombe katika mti au kichaka. Jike huyataga mayai 2-4.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Cherimiyo kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.