Benjamin Mkapa
| Benjamin Mkapa | |
|
|
|
| Muda wa Utawala 23 November 1995 – 21 December 2005 |
|
| Makamu wa Rais | Omar Ali Juma (1995–2001) Ali Mohamed Shein (2001-05) |
|---|---|
| mtangulizi | Ali Hassan Mwinyi |
| aliyemfuata | Jakaya Kikwete |
|
Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu,
|
|
| Muda wa Utawala 1992 – 1995 |
|
| Rais | Ali Hassan Mwinyi |
|
Waziri wa Habari na Utangazaji
|
|
| Muda wa Utawala 1990 – 1992 |
|
| Rais | Ali Hassan Mwinyi |
|
|
|
| tarehe ya kuzaliwa | 12 Novemba 1938 Ndanda, Masasi, Tanganyika |
| utaifa | Mtanzania |
| chama | |
| ndoa | Anna Mkapa |
| watoto | 2 |
| mhitimu wa | Chuo Kikuu cha Makerere Chuo Kikuu cha Columbia |
| Fani yake | mwandishi wa habari, mwanadiplomasia |
| dini | Ukristo |
Benjamini William Mkapa (amezaliwa 12 Novemba 1938) ni Rais wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1995-2005) na Mwenyekiti wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi, CCM (Revolutionary State Party).[1]
Yaliyomo |
Wasifu [hariri]
Mkapa ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere.[1] Nafasi alizoshikilia zamani ni pamoja na kuwa afisa wa utawala huko Dodoma na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu. Yeye pia aliongoza ujumbe wa Tanzania huko Marekani na alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje kutoka 1977 hadi 1980 na kutoka 1984 hadi 1990.[2]
Katika mwaka wa 1995, Mkapa alichaguliwa rais msingi wake ukiwa kwa kampeni maarufu ya kupambana na ufisadi na kwa kumuunga mkono kwa nguvu rais wa zamani Julius Nyerere [3] Juhudi za Mkapa za kupambana na ufisadi ni pamoja na kuumba jukwaa la wazi lililoitwa Tume ya Rais juu ya Ufisadi (Tume ya Warioba) na kuongeza msaada kwa Afisi ya Kuzuia Ufisadi.[3]
Muhula wa pili wa miaka 5 wa Mkapa kama Rais uliisha Desemba 2005. Katika wakati wake ofisini, Mkapa alibinafsisha makampuni yanayomilikiwa na serikali na akaweka sera za soko huru.[4] Wafuasi wake walimtetea kuwa kuvutia uwekezaji wa kigeni ungesaidia kukuza uchumi. Sera zake zilipata msaada wa Benki ya Dunia na IMF na kupelekea baadhi ya madeni ya nje ya Tanzania kufutiliwa mbali.[3]
Amekashifiwa kwa upungufu wa baadhi ya jitihada zake za kupambana na ufisadi [3] vilevile njia yake duni ya kutumia fedha. Alitumia £15 milioni kununua ndege ya kibinafsi ya kirais, vilevile karibu £30 milioni kwa vifaa vya angani vya kijeshi ambavyo wataalam waliona yalizidi mahitaji machache ya majeshi ya nchi .[5] Ilikuwa juu ya ununuzi huu wa mwisho ndipo Katibu wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza wa wakati huo Clare Short alielezea hasira ya umma, na kusababisha yeye kujulikana kama 'Mama Radar' katika vyombo vya habari vya Tanzania.
Baada ya kutoka ofisini kutokana na kukamilisha mihula miwili inayoruhusiwa, Mkapa anakumbwa na shutuma nyingi za ufisadi kati yao kujipa mwenyewe na Waziri wake wa zamani wa nishati na madini Daniel Yona "Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira" yenye faida kubwa katika Nyanda za juu za kusini mwa Tanzania bila taratibu zifuatazo. Kwa kujibinafsishia mwenyewe mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, alivunja katiba ya Tanzania ambayo haimruhusu rais kufanya biashara yoyote katika ikulu.
Aliteuliwa katika Bodi ya Wadhamini ya Chuo cha Aga Khan mwezi Novemba 2007.[4]
Marejeo [hariri]
- ↑ 1.0 1.1 [1] ^ "Benjamin Mkapa", Microsoft Encarta Encyclopedia 2001, WGBH (FM), pbs.org, ilitolewa 19-Oktoba-2009
- ↑ Benjamin Mkapa,
- ↑ 3.0 3.1 3.2 3.3 [4] ^ Bruce Heilman na Laurean Ndumbaro, "Corruption, Politics and Societal Values in Tanzania: An Evaluation of the Mkapa Administration's Anti-Corruption Efforts", Afr. J. polit. sd. (2002), Toleo 1 Nambari 7
- ↑ 4.0 4.1 [10] ^ "Mheshimiwa Benjamin William Mkapa", Bodi ya Wadhamini, Chuo cha AKU, ilitolewa 19-10-2009
- ↑ [9] ^ Gideoni Burrows, "We sell arms to Saddam's friends", New Statesman, 8 Septemba 2003
Viungo vya nje [hariri]
- Benjamin Mkapa bio katika Tume ya Afrika
| Alitanguliwa na Ali Hassan Mwinyi |
Rais wa Tanzania 1995-2005 |
Akafuatiwa na Jakaya Kikwete |
| Orodha ya Marais wa Tanzania | |
| Julius Nyerere • Ali Hassan Mwinyi • Benjamin Mkapa • Jakaya Kikwete |