Benedikto Yosefu Labre

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu alivyochorwa na Antonio Cavallucci mwaka 1795.
Mtakatifu Benedict Joseph Labré.
Kanisa la Santa Maria ai Monti alimozikwa.

Benedikto Yosefu Labre (kwa Kifaransa Benoît-Joseph Labré; Amettes, Boulogne-sur-Mer, Ufaransa, 25 Machi 1748 - Roma, Italia, 16 Aprili 1783) alikuwa Mkristo ambaye tangu ujanani alitamani sana maisha ya toba kali.

Kwa ajili hiyo aliiishi miaka mingi bila makao maalumu, akihiji kwa tabu nyingi makanisa mbalimbali akiwa amevaa nguo zilizochakaa na akila alichopewa tu, akitoa mfano bora wa ibada, hasa kwa kuabudu ekaristi.

Hatimaye alihamia Roma alipoishi katika sala na ufukara mkubwa sana.

Alitangazwa na Papa Pius IX kuwa mwenye heri tarehe 20 Mei 1859, halafu Papa Leo XIII akamtangaza mtakatifu tarehe 8 Desemba 1881.

Sikukuu yake ni tarehe 16 Aprili[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Attwater, Donald and Catherine Rachel John. The Penguin Dictionary of Saints. 3rd edition. New York: Penguin Books, 1993. ISBN 0-140-51312-4.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.