Bendera ya Gambia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Gambia

Bendera ya Gambia ni ya milia mitatu sambamba ya nyekundu, buluu ny kijani kibichi inyotenganishwa na kanda nyembamba za nyeupe.

Mlia wa nyekundu juu humaanisha nchi ya mbuga. Buluu chini yake ni alama ya mto Gambia unaopita nchi yote, na mlia wa kijani-kibichi ni ya misitu. Kanda nyembamba nyeupe humaanisha amani.