Bata mchovya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bata mchovya
Bata Domo-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Anseriformes (Ndege kama mabata)
Familia: Anatidae (Ndege walio na mnasaba na mabata)
Nusufamilia: Anatinae
Leach, 1820
Ngazi za chini

Jenasi 17:

Mabata wachovya ni ndege wa majini wa nusufamilia Anatinae katika familia Anatidae.

Spishi hizi hula mimea ya majini na huzamia kichwa chao tu; nyingine hutafuta chakula aghalabu ardhini.

Miguu yao iko karibu zaidi ya katikati ya mwili kuliko miguu ya mabata wazamaji na kwa sababu hiyo wanaweza kutembea vizuri. Hutokea kwa makundi kwa maji baridi au milango ya mito.

Hujenga matago yao ardhini au ndani ya shimo. Wanaweza kuruka angani vizuri na spishi za kanda za kaskazini huhamia kusini kila majira ya baridi.

Uainisho wa Anatinae hauna hakika. Hapa jenasi kumi zimewekwa ndani ya familia ndogo hii zilizopo bado, na pia jenasi tatu zilizokwisha sasa. Visukuku vya spishi ndogo vimefunuliwa katika kisiwa cha Rota (Visiwa vya Mariana) ambayo inafanana na jenasi Anas.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bata mchovya kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.