Barafu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Barafu ya mto.
Maporomoko ya mto mdogo yaliyoganda mlimani.

Barafu ni maji yaliyoganda. Maji huganda yakishikwa na baridi na kufikia 0 °C.

Barafu inaeleweka ni maji ya mgando. Hata kiowevu kingine kinaweza kushika baridi na kuganda kuwa barafu, ila kama maziwa yanaganda tunayaita "barafu ya maziwa". Pia hewa ya kaboni inaweza kugandishwa na kuwa barafu kavu.[1]

Siwa barafu katika Atlantiki ya Kaskazini.

Inapatikana katika hali na ukubwa mbalimbali. Kama ni ndogo ni fuweli kadhaa tu; kubwa zaidi ni vipande vya mvua ya mawe. Barafu inaweza kuwa ganda kubwa kama bapa nene sana kama lile linalofunika bara la Antaktiki.

Barafu ina kazi muhimu katika hali ya hewa duniani. Hasa maganda ya barafu kwenye ncha za dunia yanatunza sehemu kubwa ya maji matamu yaliyopo.

Maji yakiganda hupanuka. Hivyo barafu yake inahitaji nafasi kubwa kuliko maji ya kiowevu kiasi cha 9%. Mfano wake ni: chupa ya soda katika friji inaweza kupasuka. Sababu yake ni: maji ndani ya soda inahitaji nafasi kubwa kuliko soda ya majimaji, hivyo kupasua chupa yenyewe.

Kutokana na hali hiyohiyo, barafu ni nyepesi kuliko maji, hivyo hubaki juu ya maji. Vipande vikubwa vya barafu vikiyeyuka na barafu ya Antaktiki au Aktiki vinaelea baharini kama siwa barafu vinaweza kuharibu hata meli kubwa, jinsi ilivyoonyesha mfano wa meli Titanic.

Kwenye mtelemko wa milima barafu inaweza kutambaa kama mto ikiitwa barafuto.

marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Barafu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.