Bali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bali_Indonesia_Pura-Tanah

Bali ni kisiwa cha Indonesia. Kiko katikati ya kisiwa cha Jawa upande wa magharibi na kisiwa cha Lombok upande wa mashariki. Eneo la kisiwa ni km² 5614. Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Denpasar. Mwaka wa 2010 idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa milioni 3.89. Watu wakaao Bali huongea Kimalay cha Bali ama Kiindonesia kama lugha yao ya kwanza, na wengine wengi huvitumia kama lugha za mawasiliano.

Bali imekuwa na watu tangu Zama za Mawe za Kale. Kuanzia karibu 3000 KK, utamaduni Wa Neolithic uliibuka, unaohusishwa na wimbi jipya la wakazi ambao walileta teknolojia za kilimo cha mchele na lugha za Kiaustronesia.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]