Bahari ya Aktiki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bahari ya Aktika)
Ramani ya Bahari ya Aktiki
Dubu nyeupe huishii katika eno la Aktiki

Bahari ya Aktiki (Aktika) ni bahari inayozunguka ncha ya kaskazini. Ni sehemu ya eneo la Aktiki. Wataalamu wengine huitazama kama bahari ya pekee lakini wengine huona ni bahari ya pembeni ya Atlantiki. Kina kikubwa kiko karibu na visiwa vya Spitzbergen chenye mita 5,608.

Bahari ya Aktiki iko kati ya pwani za Asia ya Kaskazini, Alaska na Kanada katika Amerika ya Kaskazini, Greenland na Skandinavia (Ulaya). Eneo lake ni 14.056 km². Kati ya Greenland na Skandinavia kuna uwazi kubwa unaojifungua kwa Atlantiki ya Kaskazini na mlango wa Bering unaunganisha bahari hii na Pasifiki.

Sehemu kubwa ya eneo lake hufunikwa na barafu yenye unene wa mita 3 lakini sehemu hii imeanza kupungua kutokana na kupanda kwa halijoto duniani.

Mito muhimu inayoingia ni Ob, Yenissei, Lena na Kolyma upande wa Siberia (Urusi) halafu mito ya Yukon na Mackenzie upande wa Amerika ya Kaskazini.

Bahari za pembeni[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.