Eliewaha Mshana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Askofu Eliewaha E.Mshana)
Makala hii kuhusu "Eliewaha Mshana" ni fupi mno. Inahitaji kupanuliwa mapema.

Eliewaha E. Mshana alikuwa ni mwanzilishi wa Dayosisi ya Pare, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania na askofu wake wa kwanza.

Dayosisi ya Pare ilizaliwa kutoka Dayosisi ya Kaskazini ambayo ilikuwa inaongozwa na Marehemu Askofu Stephano Moshi.

Kabla kuwa askofu Mshana alikuwa mwalimu wa theolojia na mkuu wa Chuo cha Theolojia Makumira ya KKKT hadi 1972.

Katika nafasi yake ya uaskofu alisisitiza tofauti kati ya dini na siasa wakati viongozi wengine wa makanisa ya Tanzania walielekea kuunganisha wito wa kanisa na wito wa siasa ya Nyerere. [1]


Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Tumewekwa Huru – Matafakuri ya Waraka kwa Wagalati, na Mshana Eliewaha E., Central Tanganyika Press 1979 140 p
  1. Frieder Ludwig: Church and State in Tanzania: Aspects of Changing in Relationships, 1961-1994, uk. 122; via google books 6-9-2014; akirejea mchango wa E.E. Mshana "Church and State in the Independent States in Africa", Africa Theological Journal, (5/1972, pp46-58), p.49
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Eliewaha Mshana kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.