Korongo (Ciconiidae)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Anastomus)
Korongo
Korongo domo-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Ciconiiformes (Ndege kama korongo)
Familia: Ciconiidae (Ndege walio na mnasaba na korongo)
Gray, 1840
Ngazi za chini

Jenasi 6 na spishi 19:

Korongo hawa ni ndege wa familia ya Ciconiidae wenye domo refu na nene (korongo wa familia ya Gruidae wana domo fupi na jembamba zaidi). Wanaitwa kongoti pia, hususa korongo mfuko-shingo. Mabawa yao ni marefu sana, yale ya korongo mfuko-shingo yana m 3.2: marefu kuliko yale ya ndege wote ghairi ya tumbusi wa Andes (Andean condor).

Spishi nyingine huishi mahali pa majimaji nyingine mahali pakavu. Hula vyura, samaki, wadudu na nyungunyungu, hata ndege na wanyama wadogo. Korongo hawa hawawezi kutoa sauti. Lakini kwa tago hupiga kelele na domo yao.

Spishi wa Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi wa mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]