Alliance for Democratic Change

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Alliance for Democratic Change (ADC) ni chama cha kisiasa nchini Tanzania. Chama kimesajiliwa rasmi mnamo mwaka wa 2012.

Chama hiki kimejengwa katika misingi imara ya utu, uchaji wa Mungu na demokrasia ya haki. Ni chama ambacho kinalenga kuwajenga viongozi waadilifu kwa manufaa ya taifa kwa vizazi vyote.

Tofauti na vyama vingine nchini, ADC kinatambua na kuheshimu uwepo wa Mwenyezi Mungu. Huu ni mmoja ya misingi mikuu ya uongozi ndani ya ADC.

ADC inaamini kiongozi wenye kumcha Mungu atakuwa mwadilifu na mwenye kutenda haki kwa wananchi. [1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]