Adalbert wa Magdeburg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Adalbert wa Magdeburg

Adalbert wa Magdeburg (alifariki 20 Juni, 981) alikuwa mmisionari na askofu mkuu wa kwanza wa mji wa Magdeburg, Ujerumani.

Tangu kale ametambuliwa kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 20 Juni[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Adalbert alizaliwa Ujerumani na kuwa mtawa katika monasteri ya Wabenedikto wa mji wa Trier.

Baada ya kuwekwa wakfu kama askofu, mwaka 961 alitumwa mjini Kiev (Ukraine) kama mmisionari.

Kundi lake lote liliuawa, naye peke yake aliweza kurudi Ujerumani.

Baadaye aliteuliwa kuwa askofu mkuu wa dayosisi ya Magdeburg.

Alianzisha madayosisi mapya mengi upande wa Mashariki wa Ujerumani, kama katika miji ya Naumburg, Meisen, Merseburg, Brandenburg, Havelberg, na Poznan.

Mwanafunzi wake mmoja aliyetangazwa kuwa mtakatifu kama yeye ni Adalbert wa Praha.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.