Abedi Amani Karume

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Abeid Amani Karume)
Rukia: urambazaji, tafuta
Abedi Amani Karume

Sheikh Abeid Amani Karume alikuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar. Alizaliwa mwaka 1905 na kufariki tarehe 7 Aprili, 1972 kwa kupigwa risasi.

Karume aliongoza mapinduzi yaliyomwangusha Sultani aliyekuwa akitawala Zanzibar hapo mwaka 1964. Baada ya miezi mitatu Zanzibar iliungana na Tanganyika iliyokuwa ikiongozwa na Mwalimu Nyerere. Baada ya muungano wa nchi hizi mbili uliozaa jina la Tanzania, Karume alikuwa makamu wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amani Abeid Karume, ambaye ni mtoto wa Sheikh Karume, ndiye rais wa sasa wa Zanzibar tangu mwaka 2000.


Alitanguliwa na
Nafasi ilivyoundwa
Makamu wa Rais wa Tanzania
1964-1972
Akafuatiwa na
Mwinyi Aboud Jumbe
Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine