2012 DA14

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sehemu ya karibu ya dunia ya obiti ya 2012 DA14 wakati wa Februari 2013

2012 DA14 ni asteroidi lenye mzingo wa kukaribia dunia.

Imekadiriwa kuwa na kipenyo cha mita 50 na masi ilikadiriwa kuwa tani 190,000.

Kutambuliwa

Astroidi hii ilitazamiwa mara ya kwanza mwaka 2012 na wanaastronomia kwenye paoneaanga pa La Sagra. Hapo mwanzoni kulikuwa na hofu ya kwamba asteroidi hii inaweza kuwa na hatari maana kama ingegongana na dunia ingesababisha hasara nyingi sawa na nguvu ya bomu ya kinyuklia jinsi ilivyotokea mwaka 1908 huko Tunguska. [1]

Mpito wa Februari 2013

2012 DA14 ilipita karibu na dunia tarehe 15 Februari 2013 kwa umbali wa kilomita 27,700 yaani ndani ya obiti ya Mwezi na hata ndani ya obiti ya satelaiti za mawasiliano. [2]

Jinsi ilivyotabiriwa na wataalamu iilipita salama bila hatari ya muanguka chini na kugonga dunia. Hata hivyo mpito wake ulikuwa mpito wa karibu kabisa wa gimba lenye ukubwa wake ulioweza kupimwa..

Mpito ujao wa karibu utatokea mwaka 2046 lakini unatabiriwa kuwa na umbali zaidi kuliko mwaka 2013.

Ona pia

Marejeo

  1. I. Wlodarczy: The potentially dangerous asteroid 2012 DA14. Monthly Notices of the Royal Astronomical Society. Volume 427, Issue 2, kurasa 1175–1181, December 2012. Nukuu: For H = 24.377 and an albedo of 0.20 for S-type and 0.04 for C-type asteroids, we find the diameter of 2012 DA14 to be between 40 and 89 m, respectively. The JPL NASA lists H = 24.377 and D = 45 m and the NEODyS lists H = 24.4 with 30 < D < 80 m, respectively, for an albedo of 0.15. doi:10.1111/j.1365-2966.2012.22034.x
  2. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2015-04-06. Iliwekwa mnamo 2013-02-17.

Viungo vya Nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: